MAFINGA YETU BLOG

MAFINGA YETU BLOG

Breaking News
Loading...

Latest Post

Sunday, March 20, 2016

HAKIMU AKAMATWA NA TAKUKURU AKIPOKA RUSHWA TSHS 250,000

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imemkamata Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo ya Ngarenairobi Wilaya ya Siha, Gustavu Mallya (31), akituhumiwa kuomba na kupokea rushwa ya Sh. 250,000 ili atoe dhamana kwa mshtakiwa mmoja anayekabiliwa na kesi ya jinai.
Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Valentino Mlowola.
Kamanda wa Takukuru mkoani Kilimanjaro, Alex Kuhanda alithibitisha kukamatwa kwa Hakimu huyo, baada ya kuwekewa mtego na maofisa uchunguzi wa taasisi hiyo.
“Huyu Hakimu Mallya alikuwa ameomba rushwa ya Sh. 300,000 kwa mshtakiwa mmoja, ambaye alikuwa akikabiliwa na kesi ya wizi pamoja na shambulio la kudhuru mwili," alisema Kuhanda.
"Lakini alipewa Sh. 250,000 baada ya makubaliano na ndugu wa mshtakiwa na kisha akatoa dhamana hiyo."

Wednesday, February 17, 2016

NECTA:HAYA HAPA MATOKEO KIDATO CHA NNE 2015

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
 

Tuesday, February 9, 2016

Mbuzi Na Kondoo 200 Wakatwakatwa Mapanga Wakituhumiwa Kuvamia Shamba La Mkulima Huko Mvomero Morogoro



Zaidi ya Mbuzi na kondoo 200 huko Dihinda mvomero Mkoani Morogoro wamekatwa katwa na walinzi wa jadi kutoka Gairo wanaojulikana kwa jina la Mwanu ' 
 
Taarifa zinadai kuwa mifugo hiyo ilikula nusu ekari ya mazao ya mkulima mmoja kijijini hapo na taarifa zikawafikia walinzi hao ambao walifika na kukatakata mifugo hiyo mali ya mama mmoja mjane mfugaji wa jamii ya kimasai
 
Lakini Inadaiwa kuwa mifugo ya mama huyo haikuhusika kula mazao hayo bali ni mifugo ya mfugaji mwingine.
 
Waziri mwenye dhamana kupitia wizara ya mifugo na kilimo hivi sasa ameelekea eneo la tukio .

mpya:Taarifa Kwa Umma Kutoka Ofisi Ya Makamu Wa Rais


...

Friday, January 15, 2016

HAYA HAPA MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2015/2016

Sunday, January 10, 2016

magazeti ya leo jumatatu tarehe 11.1.2016

Saturday, January 9, 2016

magazeti ya leo jumapili january tarehe 10.1.2016






















 

IDADI YA WASOMAJI